Siku chache baada ya msanii wa filamu Bongo, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’
kunaswa kwenye mtego wa kujiuza, sasa ameamua kubadilisha mfumo wa
maisha aliyokuwa akiishi zamani na kuwa na mwingine mpya.
Akiongea na mwandishi wa habari hii, Aunty Lulu alifunguka kuwa kwa sasa ameamua kubadilika kwani kama ni
starehe amefanya sana pamoja na uchafu mwingi ila kutokana na mtego wa
kujiuza kumnasa na ushauri aliopewa na familia yake, amebadilika na sasa
amegeukia kwenye ujasiriamali.
“Yaani kutokana na mtego wa kujiuza nimeamua kubadilika kwa sababu jamii
ilinichukulia tofauti sana hivyo nikaamua kufanyia kazi ushauri wa
familia yangu niliokuwa nikipewa kila siku lakini nikawa naukataa.
Kwa sasa nafanya ujasiriamali na ninafurahia maisha haya kuliko yale niliyokuwa nikiishi zamani.
Aunty Lulu kwa sasa anamiliki duka la vipodozi na ni wakala wa kutoa na
kuweka fedha kwa kupitia mitandao ya simu za mkononi maeneo ya
Kinondoni Kanisani, Dar ambapo ndipo anashinda kwa sasa na kwa mujibu
wake ameachana kabisa na kujiachia kwenye sehemu za starehe na kufanya
mambo yasiyotakiwa katika jamii.
No comments:
Post a Comment