Shabiki
wa Yanga ambaye jina lake halijapatikana alikatwa kidole baada
ya jazba kati ya washabiki wa timu za Yanga na Simba zilizopelekea
Mashabiki hao kuchapana makonde leo kabla ya mechi kuanza.Tukio hilo
lilitokea katika eneo la Mwembe Yanga.
Timu ya Yanga imeonyesha ubingwa kwa kuichapa timu ya Simba mabao 2
kwa 0 huku vituko na vioja vingi vikijili uwanjana ikiwepo kichapo kwa refa..
Simba SC
: Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Haruna
Shamte, Shomari Kapombe, Mussa Mudde, William Lucian, Mwinyi Kazimoto,
Abdallah Seseme, Mrisho Ngassa, Amri Kiemba na Haruna Chanongo. Sub:
Abel Dhaira, Miraji Adam, Ramadhan Singano ‘Messi’, Felix Sunzu,
Christopher Edward, Jonas Mkude na Hassan Mkude
Yanga FC : Ally Mustapha ‘Barthez’, Mbuyu Twite,
David Luhende, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kelvin Yondan, Athuman Idd
‘Chuji’, Simon Msuva, Frank Domayo, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza na
Haruna Niyonzima. Sub: Said Mohamed, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nurdin
Bakar, Nizar Khalfan, Said Bahanuz na Jerry Tegete
Ndani ya dakika 8 za mwanzo katika kipindi cha kwanza, vijana wa Jangwani walifanikwa kumchapa Simba SC bao 1. Bao hilo lilipachikwa na Didier Kavumbagu
Baadaye Mshambuliaji
Hamis Kiiza aliipatia Yanga bao la 2 dakika ya 63 baada ya piga
nikupige katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam
PAMOJA
NA KUMCHINJA MYAMA KATIKA MECHI HIYO YA KUTIMIZA WAJIBU (YANGA
WALISHATANGAZWA MABINGWA SIKU KADHAA ZILIZOPITA), YANGA PIA IMEKABIDHIWA
KOMBE LAKE LA UBINGWA MBELE YA UMATI WA WATAZAMAJI 60,000 WALIOFURIKA
UWANJANI HAPO.
HII NI MARA YA 24 KWA YANGA KUIFUNGA SIMBA WAKATI SIMBA IMEWAFUNGA YANG MARA 19. ILA HADI SASA SIMBA INAONGOZA KWA KUIFUNGA YANGA KWA MABAO MENGI, IKIWA NI PAMOJA NA 6-0 NA MABAO 5-0 AMBAYO BADO YANGA HAWAJAJIBU MAPIGO.
HII NI MARA YA 24 KWA YANGA KUIFUNGA SIMBA WAKATI SIMBA IMEWAFUNGA YANG MARA 19. ILA HADI SASA SIMBA INAONGOZA KWA KUIFUNGA YANGA KWA MABAO MENGI, IKIWA NI PAMOJA NA 6-0 NA MABAO 5-0 AMBAYO BADO YANGA HAWAJAJIBU MAPIGO.
No comments:
Post a Comment