Ni vigumu kuamini, lakini ukweli ni
kwamba Mr.Nice ameirudia tena ile tabia yake ya Ukicheche na
kuwapanga wanawake mithiri ya vyombo kabatini iliyomfanya afulie
na hatimaye kuwa omba omba.....
Taarifa toka nchini Kenya ambako kwa
sasa msanii huyo yupo huko ni kwamba, Mr. Nice kwa sasa alala
baa akiwa amezungukwa na warembo kadhaa wanaojua kuzitumia
pesa...!!!!
Nice amekuwa akionekana katika mitaa
kadhaa ya jiji la Nairobi akiwa na "mabodigadi wa kike" ambao
amejitolea kuwadhamini LUNCH, DINNER na MATANUZI mengine...
Hongera kwa moyo wa upendo Mr.
Nice...Tunajua kwamba si vizuri tukakupangia matumizi ya pesa
yako, lakini tunakuonea huruma maana historia yako tunaijua tangu
enzi zile ulipokuwa ukitamba na nyimbo zako za "Kikulacho ki
nguoni mwako" kabla ya kufilisiwa na akina dada wa mjini....
Credit:kenyan daily post
Credit:kenyan daily post
No comments:
Post a Comment