Saturday, May 25, 2013

BOMU LALIPUKA NA KUWAJERUHI WANAFUNZI 7 WA NABOTI SEKONDARI HUKO IRINGA


 Baadhi ya Maeneo walimo jeruhiwa wanafunzi hao na Mmoja kupatwa na Mshtuko wa Mlipuko wa Mabaki ya Mabomu hayo kutokana na Tatizo lake la Moyo alilonalo na hivyo kupelekea wanafunzi Watano kulazwa Ilembula Hospitali.


 Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba akiwajulia Hali wanafunzi hao katika Hospitali ya Lutherani ya Ilembula.


 Mwanafunzi Evance Joseph[16]kidato cha Kwanza ambaye alikuwa akifanya Majaribio ya Kuchoma Mabaki hayo ya Bomu huku Mengine akiyahifadhi kwenye Tranka lake la Nguo.


 Wanafunzi wakiwa wanaendelea kufanyiwa Vipimo vya Mionzi ya Jua kutambua ukubwa wa Tatizo  katika Hospitali ya Ilembula Wilayani Wanging'ombe Mkoani Njombe.


 DC Njombe na Msafara Wake wakiwatazama Wanafunzi waliojeruhiwa na Mabaki ya Mabomu hayo.


 Hapa Mkuu wa Wilaya na Msafara wake ukiongozwa Na JWTZ Makambako.


 Msafara ukiwasili katika Shule ya Sekondari NABOTI Iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Makambako.



 Wanafunzi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Njombe.


 Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari NABOTI Mara baada ya kutoka katika Hospitali ya Ilembula kuwajulia Hali wanafunzi Watano waliolazwa kwa Matibabu.


 Wanafunzi wa NABOTI Sekondari wakimsikiliza DC na Msafara wake.


 
Wanafunzi Wanne wa shule ya sekondari NABOTI iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Makambako wamejeruhiwa na Mlipuko wa Mabaki ya Bomu huku mmoja akipata Mshtuko wa Moyo kutokana na Mlipuko huo Baada ya Wanafunzi Takribani saba wa Kidato cha Kwanza kwenda kuyaokota Mabaki hayo kwenye Mlima uliopo Jirani na maeneo ya Jeshi.

No comments:

Post a Comment