Saturday, May 25, 2013

WANASHERIA WAAPA KUWASHITAKI WASANII WA KUNDI LA ZE KOMEDY KWA KUWADANGANYA WASICHANA WAPIGE NUSU UCHI ILI WAWE MASTAA



Zile picha za kundi la Ze Komedy la linalorusha kipindi chake kupitia televisheni ya East Africa TV zinazowaonesha wasanii hao wakiwa na mabint ufukweni zimechukua sura mpya baada ya wanasheria  kuahidi kuzisaidia familia za wazaza wa mabint hao.

Wakitoa maoni yao kwa nyakati tofauti, wananchi hao wamesema" Nimeziona picha hizo kupitia mtandao wenu kweli imeniuma kama mzazi kwani huo ni unyanyasaji ambao haukubariki hata kidogo naziomba familia za mabint hao kuchukuwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kushtaki ili iwe fundisho kwa wasanii wengine wanaopenda kudhalilisha watu wengine kwa masrahi yao binafsi" Alisema Fortunatus Kasomfi ambae ni mtanzania anaeishi nchini Afrika Kusini

Aidha nae Hawamu Juma ambae ni mkazi wa Arusha maeneo ya Unga Limited ambae ni Mwanasheria maarufu Mkoani humo alioneshwa kusikitishwa sana na tukio na kuwashauri wazazi wa wasichana hao kumtafuta kwa ajili ya kuwafungulia mashtaka wasanii hao
 
" Napenda kuwashauri wazazi wa wabinti hao kama wanahitaji msaada wa kisheria wanitafute kupitia  simu namba 0713-146416 nitawapa mawazo ya kitaalam ya kisheria ili wasanii hao wafikishwe mahakamani" Alisema Mwanasheria huyo

Taarifa  za  ndani ya chungu zinadai  kuwa  kulikuwa na ushawishwaji mkubwa kwa mabinti hao wakati wa kupigana picha hizo kwa madai kuwa watasaidiwa kuwa mastaa kama watapiga picha hizo na mastaa hao. 
Huyu  ni  Happy na Master  Face  wakifanya  Uchafu wao....Hapa  wanatomasana  kabla ya uzalendo kuwashinda  na  kuamua  kuvunja  amri  ya  sita...


 
Tayari kuna taarifa kuwa baba mzazi wa mmoja wa wasichana hao ambae anaishi Tabata ameanza kuchukuwa hatua za awali kwani siku ya tukio msanii wa kundi la Komedy Manaiki Sanga alifika nyumbani kwa bint huyo na kumchukuwa kwa madai kuwa anaenda nae Location.

Mpaka sasa kiongozi wa kundi hilo ambaye  ni Mtanga ameshindwa kuchukuwa hatua yoyote dhidi ya wasanii wake walihusika na tukio hilo chafu ....

No comments:

Post a Comment