Monday, April 29, 2013

MWANAUME AZIKWA AKIWA HAI JIJINI MBEYA KWA MADAI KUWA NI MCHAWI


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida wananchi wa kijiji na kata ya Mkwajuni Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya  wamemzika Mwanakijiji mwenzao akiwa hai wakimtuhumu kusababisha kifo cha Mkazi mmoja kijijini hapo. 
 
Tukio hilo la kusikitisha limetokea Apri 26 mwaka huu majira ya Saa Nane Mchana katika Kitongoji cha Maweni Makaburini baada ya Mhanga aliyefahamika kwa jina la Victory Mwachirui(68) kuhudhuria mazishi ya Pita Barton(28)aliyefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.

 
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Thobias Ismail amesema marehemu alipatwa na mauti akiwa anapatiwa matibabu kwa mganga wa jadi ambaye jina lake halikuweza kujulikana maramoja.


Amesema wakati taratibu za mazishi zikiendelea Ndugu wa marehemu walidai kuwa kifo cha Marehemu kilisababishwa na Mwachirui ambaye ni Katekista mstaafu kwa imani za kishirikina.


Ameongeza kuwa wakati kaburi likichimbwa kwa ajili ya kumzika marehemu ndipo vijana waliokuwa wakichimba waliagiza Wazee wa Mila wafike makaburini kwa ajili ya kuangalia utaratibu wa mazishi na kukagua ukubwa wa Kaburi ambalo lilikuwa limekwisha chimbwa.



Kutokana na mwito huo walifika wazee wanne akiwemo Mzee Mwachirui ambaye walimsisitiza kusogea jirani na kaburi ambapo baada ya kusogea alipigwa na Sururu kichwani na kuangukia kaburini huku akisindikizwa na marungu..

Jeneza la aliyekufa kwa ugonjwa tayari limetolewa pembeni. Sasa anafukuliwa aliyezikwa akiwa hai
Jeneza la aliyekufa kwa ugonjwa tayari limetolewa pembeni. Sasa anafukuliwa aliyezikwa akiwa hai

                     Mwili wa aliyezikwa hai unatolewa kaburini 
Mwili wa aliyezikwa hai unatolewa kaburini

                     Dada wa marehemu aliyezikwa akiwa hai
Dada wa marehemu aliyezikwa akiwa hai

No comments:

Post a Comment