Thursday, May 16, 2013

"NATAKA GODBLESS LEMA AJE AJISAFISHE HUKU LONDON KAMA KWELI HAKUBAKA".... CHRIS LUKOSI



Ndugu zanguni,

Baada ya kuona kila kukicha tunaendelea kusikia hizi habari zenye kukera kuhusu kesi inayomkabili mbunge wa Arusha God bless Lema.

Mimi kama rafiki wa zamani wa Lema nimeamua kujitolea kumplipia gharama zote ili aje hapa UK kukanusha uzushi huu ambao ni aibu kwa taifa letu kuwa na mbunge ambaye anatafutwa kwa kesi ya aibu ya kubaka.

Mimi kama wananchi wengine sipendi kuona jina la mheshimiwa lina chafuliwa hivyo nimeamua kuwa nitalipa kila kitu kuanzia tiketi ya ndege, ada ya visa na pia gharama za hoteli, chakula na vinywaji kwa kipindi chote mheshimiwa atakapokuwa hapa.

by Chris Lukosi( Alikuwa mwenyekiti wa chadema london)

No comments:

Post a Comment